... helping you be all that God made you to be, because He plans on shining His light into this world through you.

Berni - ceo, Christianityworks

Msingi wa Utakatifu

We're glad you like it!

Enjoying the content? You can save this to your favourites by logging in to your account.

Register or Login

Add to Favourites

Waebrania 12:14 Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao.

Listen to the radio broadcast of

Msingi wa Utakatifu


Download audio file

Acha nikuuliize leo swali la tafakari kidogo halafu unijibu.  Je!, Kipaumbele kilichopo maishani mwako ni kipi?  Eeh, vipaumbele ndivyo vinavyomwongoza mtu katika maisha yake.

Kama hatuchunguzi vipaumbele vyetu mara kwa mara, tutajikuta tunaishi katika mazoea tu bila kufikiria, na ni ajabu kuona namna maisha yanavyokwenda kasi.

Kipaumbele changu cha kwanza ni kumheshimu Mungu.  Kila asubuhi natafakari hilo na kuliombea.  Bado inanishangaza mno jinsi Yesu alivyokufa kwa ajili ya dhambi zangu.  Kwahiyo; ninampenda, ninataka kumheshimu na ninataka kumwishia.  Ndivyo nilivyo mimi.  Wewe, je!  Ni kipi kinachotanguliza orodha ya vipaumbele vyako?

Kama tulivyoona siku chache zilizopita, ni baraka kubwa kujua kwamba hatuhitaji kujaribu kutimiza lengo hilo kwa kutumia nguvu zetu.  Mtu akimwamini Yesu, Mungu anampa Roho yake, Roho Mtakatifu, ili amsaidie kusafisha mwenendo wake kama vile wanatheolojia wanavyosema, “kumtakasa”…kumfanya awe mtakatifu.

Lakini; na sisi tuna sehemu katika zoezi hili; ni kumheshimu Mungu; na  kufanya ule “utakatifu” kuwa kipaumbele chetu cha kwanza kabisa.  Huu ndio utofauti kati ya mwamini na mwanafunzi; kati ya mtu anakubali kwa kichwa kwamba Yesu alikufa kwa ajili yake.. na yule anayemwishia yeye kwa moyo wake wote.

Waebrania 12:14  Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao.

Ina maana, weka utakatifu kuwa kipaumbele maishani mwako; weka kumheshimu Mungu kuwa kipaumbele maishani mwako; weka kuishi na kutembea na hata kuvuta pumzi kwa ajili yake – kuwa kipaumbele chako cha kwanza.

Utakatifu – utakatifu wako – ni ushirikiano.  Hauhitaji kuutafuta peke yako, lakini bado unahusika kwa sehemu kubwa. 

Hili ndilo Neno la Mungu safi na lenye afya kwa ajili yako leo.


We use cookies to improve your browsing experience, analyse site traffic & personalise content, but we do not track you when you leave this site. To find out how we utilise & protect your data, check out our "Privacy Policy".

Privacy Policy